Akijibu swali katika kikao cha baraza la wawakilishi kwa niaba ya
Waziri,Naibu Waziri wa kazi,Uwezeshaji,Vijana,Wanawake na Watoto Shadia
Muhammed Suleiman amesema kutokana na wananchi kuunga mkono juhudi za
serikali katika kupiga vita ajira za utotoni serikali imefanikiwa
kuwarejesha skuli Baadhi ya watoto waliokuwa wanajishughulisha na kazi
hizo.
Hata hivyo amesema kutokana na baadhi ya wananchi kushindwa kudhibiti
watoto wao kujiingiza na vikundi hatarishi ikiwemo ajira za utotoni
wizara hiyo pia imeandaa mpango maalumu wa utoaji elimu ya kupambana na
ajira hizo ili kuhakikisha watoto wanapatiwa haki zao za Msingi.
Kwa mujibu wa kauli za Wizara hiyo zaidi ya watoto elfu tano wa
Wilaya 11 za Zanzibar waliokuwa wanajishughuliza na Ajira za utotoni
wamerejeshwa skuli ili kuendelea na masomo yao.
chanzo;zanzibar24.
Comments