Akijibu swali katika kikao cha baraza la wawakilishi huko chukwani
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mmanga Mjengo Mnawiri
amesema kwa kipindi kirefu skuli za Zanzibar hususani Mkoa wa Mjini na
za Shamba zinakabiliwa na tatizo hilo na kupelekea wanafunzi kukosa haki
zao za msingi.
Katika kulipatia Ufumbuzi tatizo hilo Wizara inaendelea na hatua ya
kuwaajiri walimu wa masomo ya Sayansi na hisabati pamoja na masomo ya
kingereza,Historian a Jiografia ili kuondoa usumbufu wanaoupata
wanafunzi wakati wanapohitaji elimu.
Wakati huo huo akijibu suali la nyongeza kuhusu mpangilio mbaya wa
mishahara pamoja na Posho wanazodai walimu kwa shughuli mbalimbali
ikiwemo posho za likizo na kusainisha mitihani ya wanafunzi amefahamisha
kuwa tatizo hilo limeanza kuchukuliwa hatua za awali ambapo walimu hao
watalipwa kwa awamu.
chanzo;Zanzibar24
Comments