Rais wa Zanzibar kusaini Mswada wa Mafuta na Gesi Asilia kesho..

ALI-MOHAMED-SHEIN-1Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mheshimiwa Dkt. Ali Mohammed Shein kesho tarehe 15/11/2016 saa 4.00 asubuhi atasaini Mswada wa Sheria ya uchimbaji mafuta na gesi asilia wa mwaka 2016, Ikulu Mjini Zanzibar.

Mheshimiwa Rais Dkt. Shein atasaini Mswada huo wa Sheria baada ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar kuupitisha katika mkutano wa tatu wa Baraza hilo lililofanyika mwezi Septemba mwaka huu.

Mheshimiwa Rais atasaini mswaada mbele ya waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari vya hapa nchini.

Kutiwa saini mswada huo hapo kesho kutawezesha kazi ya utafutaji na uchimbaji wa mafuta na gesi asilia Zanzibar kuanza katika visiwa vya unguja na pemba.
mswada mafuta na gesi zanzibar 
chanzo; zanzibar24.

Comments