Alisema anayodhamira ya kweli ya kuondoa kero, changamoto na
malalamiko yanahusua Muungano huo, akiamini kuwa kama hilo litafanyika,
linaweza kuimarisha maisha ya wananchi wa pande zote.
Waziri Makamba ameeleza hayo, ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini
Pemba, mara baada ya kupokea taarifa ya kazi ya mkoa huo, kwenye ziara
yake fupi ya kuangalia jengo la Ikulu la Makamu wa rais wa Jamahuri ya
Muungano wa Tanzania yalililopo mjini Wete.
Alisema kufanya hivyo, ndio malengo na dhamira za serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar na ile ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, katika
kuweka sawa kero za Muungano.
Aidha Waziri huyo alisema, ndio maana wanaangalia uwezekano mkubwa wa
kulifanyia matengenezo makubwa jengo la Ikulu kwa ajili viongozi wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ili wanapofika kisiwani Pemba wawe na
makaazi ya uhakika.
“Mimi nisema umoja wetu huu uliopo baina ya serikali zetu mbili,
utaimarika zaidi ikiwa kero na malalamiko ya Muungano kwa pande zote
zitatuliwa’’,alifafanua.
Waziri huyo alisema jambo lililofanywa na Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar, kukabidhi jengo hilo kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano, ni
faraja na sasa wanajipanga ili kuliimarisha.
Alisema katika ziara yake hiyo, amefuatana na timu ya wataalamu
kadhaa wakiwemo wakala wa majengo, ili kufanya tathimini na kuwa na
gharama halisi, ili kuangalia bajeti ijayo kama wataweza kuingiza fedha.
Kuhusu uwepo wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, baada ya uchaguzi
wa marudio, Waziri Makamba, alisema ipo kihalali na kisheria na wala
hakuna mwenye ubavu wa kuiondoa.
Alisema Dk Shein, ni rais halali kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar ya
mwaka 1984, na ataendelea kuhudumu akiwa rais wa Zanzibar, hadi uchaguzi
mwengine.
Mapema Waziri huyo amewapongeza wafanyakazi wa jengo hilo, kwa
kuendelea kulitunza ndani na nje, na kuwaahidi kuwa serikali ya Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania, italifanyia matengenezo makubwa.
Akisoma taarifa ya kazi ya Mkoa wa kaskazini Pemba, Katibu tawala wa
mkoa huo Yussuf Mohamed Ali, alisema pamoja na changamoto kadhaa
zilizopo, lakini huduma ya maji safi na salama, inapatikana kwa asilimia
88 na hasa baada ya kukamilika kwa mradi wa maji mjini na vijijini.
Aidha, alimueleza Waziri huyo kuwa tatizo la miundombinu ya barabara,
yamekaa sawa, hasa baada ya kukamilika kwa barabara tano, zenye urefu
wa kilomita 35, zilizojengwa kwa ufadhili wa Mfuko wa Changamoto ya
Milenia wa Marekani (MCC).
Mara baada ya kufanya kikao hicho cha kupokea taarifa ya kazi ya Mkoa
wa kaskazini Pemba, Waziri Makamba na ujumbe wake, ulilitembelea jengo
hilo la Ikulu kwa ajili ya viongozi wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania
mjini Wete.
chanzo;zanzibar24.
Comments