Afisa Ustawi wa Jamii aitaka Serikali kueka mkazo marufuku ya uvutaji Sigara kiholela.

sigaraAfisa ustawi wa jamii wa Tume ya kudhibiti dawa za kulevya ofisi ya Makamo wa pili wa Rais, Juma Said Seif ameishauri serikali kuchukua jitihada za upigaji marufuku uvutaji wa sigara kiholela katika mikusanyiko ya watu ili kuweza kupunguza matumizi ya dawa za kelevya nchini.

Akizungumza na Zanzibar24 amesema watu wengi wanaotumia siagra hujihusisha na matumizi mabaya ya dawa za
kelevya hali inayochangia kuongezeka idadi ya watumiaji wa dawa hizo.
 
Hata hivyo amesema Matumizi ya dawa za kulevya huongeza mzigo kwa taifa kwa kuwa hupunguza nguvu kazi na husababisha uharibifu wa mali na . gharama za udhibiti zikiwemo utoaji wa elimu kwa umma, uteketezaji wa mashamba ya bangi, uendeshaji wa kesi, kuwatunza wafungwa magerezani na kuwatibu watumiaji huongeza mzigo kwa taifa na jamii kwa ujumla.

chanzo;zanzibar24

Comments