Wananchi watakiwa kujenga utamaduni wa kutembelea sehemu za kihistoria.

kizimkazimosque
Wananchi wa Zanzibar wameshauriwa kutembelea sehemu za kihistoria zilizopo nchini ili kujifunza historia ya nchi yao na kutuza utamaduni iliopo.

Akizungumza na chanzo hiki cha habari  msimamizi wa pango la kihistoria la mwanamiza lililopo kizimkazi Ibarahim Naimu amesema Zanzibar ni sehemu iliokusanya historia mbalimbali lakini wanashangwaza na baadhi ya wazanzibar kutojuwa umuhimu wa historia hizo.

Hata hivyo amesema endapo wananchi watakuwa na utamaduni wa kutembelea sehemu mbalimbali za kihistoria ikiwemo magofu ya zamani na miskiti mikongwe watajifuza mambo mengi yatakayoibua vyanzo na kukuza uchumi

Aidha ametowa wito kwa serikali kuunga mkono juhudi za watunza sehemu hiyo ya kihistoria ya kizimkazi kwa lengo la kukuza sekta ya utalii na kuimarisha ajira kwa vijana.

chanzo; zanzibar24.co.tz

Comments