
Wananchi hao
wameyasema hayo huko kijijini kwao wakati wakizungumza na mwandishi wa habari
hizi juu ya kuwepo kwa malalamiko ya fidia waliaahidiwa kua ndogo na
kutozingati thamani ya nyumba zao.
Ali Juma Khamis
mmoja kati ya wananchi wa Vitongoji Vumba amefahamisha kua tathmini iliyofanywa
ya kulipwa fidia hizo haikidhi mahitaji ikilinganishwa na garama za viwanja kwa
sasa vimekua vya bei ya juu hasa kwa wananchi wenye kipato cha chini.
Amesema
kuwa ipo haja kwa serekali kuliangalia
upya suala hilo ili kuondokana na
usumbufu ambao unaoweza kujitokeza.
Nae Said Hassana Abdalla amesema jitihada za
maksudi zinahitaji kwa serekali katika kutathmini upya gharama hizo ili wapate sehemu za kuishi na familia zao
bila kuwepo matatizo.

Amefahamisha
kua wametoa elimu kwa jamii juu ya ujenzi wa barabara unavyo weza kuwanufaisha
watu, lakini pia nachangamoto zinapojitokeza hususan kwa wale ambao ni wageni
wa kijiji hicho huku akihimiza kulinda mila na tamaduzi za kijiji chao.
Sambamba
nahyo sheha wa shehiya hiyo Salum Ayub Suleiman ameiomba wizara husika kuchukua
hatua za haraka kurudi kijijini hapo
ilikujionea kero zilizopo kwa wananchi na kuhimiza kuwekwa matuta barabarani
pindi itakapo kamilika ili kupunguza ajali zisiszo zalazima.
Comments