
Wakizungumza
na mwandishi wa habari hizi katika mashamba yao
mkomani shehia ya vitongoji wakulima hao wamesema wamekua wakizalisha
bidhaa nyingi lakini wanashindwa kujiendeleza kutokana na ukosemu wa maji hali
ambayo inarejesha nyuma harakati zao za kilimo.
Akizungumza
kwaniamba ya wakulima wenzake Mariya Saleh Juma amesema kilimo cha kusubiria nvua kimepitiwa na
wakati kwani inaweza kupita miongo ambayo niyanvua na isinyeshe kabisa jambo
ambalo linakatisha tama ya kuendeza kilimo hicho.
Amefahamisha
kuwa licha ya kujaaliwa kuwa maziwa ya maji
lakini bado wanapata usumbufu mkubwa
wakuchota kwa ndoo hadi mashambani jambo
ambalo linawapotezea muda mkubwa, na kutofikia malengo walio jiwekea kwa haraka.
“laity kama
tungalikua na mashine za kusukumia maji kutoka kwenye yale maziwa ingekua
rahisi sana kwetu lakini yote yaha nikua hatuna vifaa, tunafanya tu ilikupata
chochote ambacho kitatusaidia katika maisha yetu”.
Aidha
amesema kuwa wamepata hasara kubwa ya kilimo chao cha matikiti, mabilingani,
tungule, mabamia na mboga mboga nyengine
kuharibika kutokana na kiangazi
na kuwasababishia hasarakubwa.

Amefahamisha
kuwa vikundivingi vya ushirika
huanzishwa na badala yake kufa kutokana na ukosewu wa dhana za kujiendezea
pamoja kukosa ruzuku hasa hasa kwa wakulima wadogo wadogo.
Nae diwani
wa wadi ya Vitongoji Abdalla Juma Abdalla amesema kuwa kuwepo kwa ajira zisizo rasmi zinachangiwa na hali ngumu za
kimaisha lakini katika wadi yao tatizo hilo limepungua kwa asilimia kubwa.
Sambamba
nayo ameiomba serekali kutoa mikipo kwa wajasiriamali wadogo wadogo ili waweze
kujiendeleza na kuondokana na hali ngumu za kimaisha.
Comments