Waziri wa serekali ya mapinduzi zanzibar wakanusha ubovu wa mezani za kununulia karafuu Kisiwani Pemba.
.jpg)
Waziri asiyekua na wizara maalum wa serekali ya mapinduzi Zanzibar
Said Sudi Said amewaomba wananchi wa Wilaya ya Mkoa kuondoa wasiwasi juu ya
tatizo la mezani wanayopimiwa karafuu, kuwa ni mbovu na serekali itaendelea
kutoa haki na hakuna mwananchi anaye ibiwa kwa njia yoyote.
Ameyasema hayo huko Mkoani
alipokua akizungumza na wauzaji wa karafuu katika kituo cha ununuzi Mkoani Mkoa
wa Kusini Pemba.
Amesema kumekuwepo na uvumia
kwa baadhi ya watu kuwa mezani ya
kupimia karafuu katika kituo cha kununulia karafuu mkoani ni mbovu, bali huwo
ni uzushi unaolenga kuzoofisha ununuzi wa zao hilo na watahakikisha kua iwapo
kuna mapungufu yoyote yanashughulikiwa.
Naye Waziri asiye na Wizara
maaluum Juma Ali Khatib amewahakikishia wakulima wa zao la karafuu kuwa
serekali haitowakopa wakulama katika mauzo ya zao hilo.
Amesema serekali inafedha za
kutosha zinazo kimu kununulia zao hilo na wala haito shusha bei na kuahidi
kuliendeleza kwa umakini mkubwa.
Sambamba nahayo mkuu wa
uchukuzi wa kituo cha Mkoani Mohd Makame Haji
( Pachingo ) amelalamikia shirika la meli ya Zanzibar kusababisha
usumbufu wakati wa kupakia karafuu kwa ajili ya kusafirishwa.
Comments