Watahiniwa Laki 7.9 kufanya mtihani elimu ya msingi

JUMLA ya watahiniwa 795,761 wanataraji kufanya mitihani yao ya kumaliza elimu ya msingi nchini (PSLE) kwa mwaka huu.

Akizungumza jijini Dar es Salaam leo, Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA), Dk Charles Msonde amesema wanafunzi hao wamesajiliwa kufanya mitihani yao Septemba 7na 8 mwaka huu.

Msonde amesema wanafunzi hao watafanya mtihani ni kiswahili, Kiingereza, Sayansi, Hisabati na Maarifa ya jamii.

Wanafunzi 763, 602 walifanya mitihani hiyo mwaka 2015 na wanafunzi 518,034 wakafaulu.

chanzo;habarileo. 

Comments