Wanchi wa kijiji cha kiziwani walalamikia tatizo la maji katika eneo lao kwa muda mrefu sasa.

Image result for pemba island
Wananchi wa kijiji cha kiziwani Shehia ya shungi Wilaya ya chake chake Pemba wameiomba Mamlaka ya Maji Zanzibar(ZAWA) kufanya juhudi za kufikisha maji safi na salama  katika kijiji hicho iliyopatikana kwa tabu hadi sasa .


 akizungumza na zenj fm Mmoja ya awakaazi wa kijiji hicho abeda Hamad amesema ni kipindi kirefu sasa wamekuwa wakipata huduma hiyo kwa tabu na siku ambayo wanapata inakuwa hayakidhi haja kutokana na kupatiwa ndoo 4 tu kwa kila baada ya siku mbili.


Kwa upande wake bi Mwamize Khamis amesema  huduma ya maji safi na salama  imekuwa ikipatikana kwa tabu  kadri ya miaka 25 hadi sasa.


Afisa uhusiano Mamlaka ya Maji Pemba Suleiman Annas Massoud amesema sababu ya kukosekana kwa huduma ya maji safi na salama katika baadhi ya vjiji ni kutokana na mtandao wa kusambazia maji kuwa mdogo ila kwa sasa mamalaka ya maji Zanzibar ZAWA imeshachimba visima 15 vitakavyoweza kueneza huduma ya maji safi na salama katika vijiji vyote ambavyo huduma hiyo inapatikana kwa tabu na sio kwa kijiji cha kiziwani pekee.


Hivyo amewataka wananchi  kisiwani pemba  kuwa na subra katika kipindi hiki mamlaka ya maji zanzibar ZAWA  ikiwa ipo katika juhudi na harakati za kufanikisha huduma ya maji safi na salama inawafikia wananchi wa mjini na vijijini bila ya usumbufu wowote.

Comments