
Katika uteuzi uliofanyika karibuni wanachama kadha wa Tamwa walipata nafasi.
Tamwa iliwataja wanachama wake na nafasi zao ni Mahfoudha Alley Hamid
(Ummie) ambaye amekuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la
Magazeti ya Serikali Zanzibar, Maryam Hamdan (Mwenyekiti wa Baraza la
Sanaa na Sensa ya Filamu na Utamaduni Zanzibar), Nasra Mohamed Juma
(Naibu Mkurugenzi wa Shirika la Utangazaji Zanzibar (ZBC) na Rahel
Mhando (Katibu Tawala Wilaya mpya ya Kigamboni).
Mkurugenzi Mtendaji wa Tamwa, Eddah Sanga alisema taasisi hiyo
inaamini kuwa, katika kuleta mabadiliko ya kimaendeleo nchini, uteuzi wa
wanawake katika nafasi za juu ni fursa itakayowezesha kuondolewa kwa
mapungufu yaliyopo kiuongozi ili kuwepo usawa na haki kwa watanzania
wote.
chanzo;habarileo.
Comments