
Rais Shein alitoa kauli hiyo juzi usiku katika harambee hiyo iliyofanyika katika hoteli ya Park Hayat visiwani hapa.
Alisema kwamba katika safari yake ya harakati za kuimba, msanii huyo
alikutwa na misukosuko mingi ikiwemo watu kumkejeli kwa wimbo na kwa
mashairi.
Hivyo alisema kwamba ujenzi wa jengo hilo utatoa fursa ya kuzidi
kutambulika kwa kazi za msanii huyo kutokana na watu wengi kufika na
kusoma historia yake na kutambua mahala alipozaliwa. Alisema kwamba wana
jukumu la kila fani nao kumtuza kutokana na mchango wake mkubwa
alioutoa katika kuipa heshima nchi yao.
“Ni wajibu wa kuitunza ajira yake na maisha yake, Siti alifanya kazi
kubwa katika kukitangaza Kiswahili na Kiswahili alichokitumia kile cha
hali ya juu katika nyimbo zake, ambapo kwa sasa hatuwezi kukipata,"
alisema.
Hata hivyo, alisema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inafanya uwazi
wa kuwaenzi waimbaji wote wakongwe na wa sasa. Siti Binti Sadi alizaliwa
mwaka 1870 katika kijiji cha Fumba, ambapo ndipo kutajengwa jengwa hilo
na kufariki dunia mwaka 1950 na kuzikwa Rahaleo.
Katika harambee hizo jumla ya sh milioni 800 zilipatikana zikiwemo ahadi, ambapo Rais wa Zanzibar akichangia Sh milioni 50.
chanzo;habarileo.
Comments