Dawasco kuondoa mita zote za maji chakavu

SHIRIKA la Majisafi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASCO) limeanza zoezi la kuondoa mita za maji zote chakavu katika jiji la Dar es salaam ili kupunguza tatizo la upotevu wa maji linaloendelea kulikumba shirika hilo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Afisa Mtendaji Mkuu wa Dawasco, Cyprian Luhemeja amesema  jumla ya mita 100,000 tayari zimeshaagizwa kwa ajili ya zoezi hilo.

“Tayari Dawasco ina mpango wa kubadilisha mita za Maji zote zenye umri mkubwa kwenye maeneo yote ya Jiji la Dar es Salaam pamoja na maeneo ya mkoa wa Pwani, ila tutaanzia na maeneo ya Magomeni, Kawe pamoja na Kinondoni kwa kuwa mita nyingi za maji huko zina umri wa zaidi ya miaka 10, “alisema Luhemeja.

Kwa habari zaidi usikose nakala yako ya Habarileo Septemba 7.

chanzo;habarileo.

Comments