Wanachama na wadau wa NOCOMPED
COMMUNITY MEDIA wametakiwa kuendeleza
mashirikiano yao walio nayo ili kutekeleza vyema majukumu ipasavyo.
Wito huo umetolewa na
mwenyekiti wa kamati ya usimamizi ya ujenzi wa kituo hicho ND. MOHD NASSOR
SULEIMAN kilichopo Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba wakati wa ziara maalum ya
kukagua hali ya ujenzi na kuweka mikakati madhubuti ya kiutendaji ndani ya jumuiya hiyo.
Amesema kila mmoja anatakiwa
kua na ham ya kujitolea kwa moyo wote ili kutoa msukumo kwa viongozi wanaosimamia
ujenzi wa kituo hicho cha radio na kukamilika kwa mudauliowekwa.
Amefahamisha kua bila ya kuwepo
kwa umoja na mashirikiano dhati ndani ya jumuiya hiyo hakuna mafanikio yoyote
ambayo yataweza kufikiwa na kurejesha nyuma maendeleo.
“ Nihakika penye umoja ndipo
penye mafanikio umoja wenu ndio utakao kuza jumuiya pamoja na kuleta maendeleo
endelevu katika kujikomboa kimaisha”.
“ siri ya maisha duniani nikua na
maashirikiano bila ya mashirikiano hakiuna mafanikio hivyo bc tuamini yakwamba
tutafanikiwa kwa mashirikiano yetu”.
Aidha ametoa wito kwa mashirika
ya kisereli nayale ya umma kuunga mkojono jitihada za wananchi pamoja na jumuia
ndogo ndogo kuzisaidia kwa hali na mali
ilikujikimu kimaisha na kuondokana na hali ya utegemezi.
Nao wadau wa jumuiya hiyo wamemuhakikishia
mwenyekiti huyo kua kwataendeleza
kuyalinda mashirikiano yao ili kufikia pale ambapo wamelenga kupafika na
kuondokana na hali ngumu ya kimaisha.
BAKAR HAMAD ABDALLA kwaniamba
ya wadau wenzake amemuomba mwenyekiti huyo kuendelea kua na moyo wa subra kwa kuendelea
kujitolea ili waweze kuyafikia kwa urahisi malengo ya ujenzi wa kituo hicho.
Amesema licha ya mafanikio
yaliyo fikiwa na jumuiya hiyo ipo haja
kwa mwenyekiti huyo pamoja na wadau wengine kuendelea kujitolea, kwani nguvu za ziada zinahitaji ili
kukamilisha ujenzi wa kituo hicho cha radio.
“ Ipohaja kwa serekali na
taasisi nyengine za umma kuungana kwa pamoja ili kukidhhi matwa na malengo
tulio jiwekea ili tuweze kukamilisha vyema kituo chetu na malengo yetu
yakamilike kwa muda muafaka”.
Comments