Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein Awaapisha Viongozi Aliowateua Ikulu leo.

AARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein leo amewaapisha Manaibu Makatibu Wakuu wawili ambao aliwateua hapo jana.
Katika sherehe hiyo fupi iliyofanyika Ikulu, Mheshimiwa Rais alianza kwa kumuapisha ndugu Hassan Khatib Hassan kuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto anayeshughulikia masuala ya Wazee,Vijana,Wanawake na Watoto.
 
Shughuli hiyo ya kiapo ilikamilika kwa Mheshimiwa Rais kumuapisha Kamishna Msaidizi wa Vyuo vya     Mafunzo (ACP) Sida Mohammed Himid kuwa Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Serikali za Mitaa, Tawala za Mikoa na Idara Maalum za SMZ anayeshughulikia Idara Maalum za SMZ.
 
Sherehe hiyo ilihudhuriwa na viongozi mbali mbali akiwemo Spika wa Baraza la Wawakilishi Mheshimiwa Zubeir Ali Maulid, Jaji Mkuu wa Zanzibar Mheshimiwa Omar Othman Makungu, Wajumbe wa Baraza la Mapinduzi, Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Mheshimiwa Said Hassan Said na Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Dk. Abdulhamid Yahya Mzee .
 
Wengine ni Mkuu wa Mkoa Mjini Maghribi Mheshimiwa Ayoub Mohamed Mahmoud, Kadhi Mkuu wa Zanzibar sheikh Khamis Haji na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Zanzibar Mheshimiwa Khatib Abdulrahman Khatib.
 
chanzo;zanzinews

Comments