Mashindano ya uhamasishaji wa lugha ya kiarabu kwa walimu wa vyuo vya kiarabu vilivyo chini ya Taasisi ya Samail yamalizika vyema.

JUMLA ya
Wanafunzi 1041 sawa na 41.85%, wamefaulu mitihani yao ya lugha ya
Kiarabu, kati ya wanafunzi 2700 waliofanya mitihani hiyo iliyosimamiwa
na Taasisi ya Samail Academy iliyopo Chake Chake Pemba.
Awali
Wanafunzi 10935 kutoka Vyuo 105 vinavyosimamiwa na taasisi hiyo, ndio
waliotarajiwa kufanya mitihani hiyo, lakini walishinbdwa kutokana na
mchujo uliokuwepo na kupatikana idadi hiyo.
Alisema mitihani hiyo iliyofanyika katika maeneo Tisa tafauti, huku ikisimamiwa na walimu na viongozi kutoka Samail Academy ili kupata wahitimu bora.
Aliyataja maeneo ambayo mitihani hiyo imefanyika ni Wingwi, Chake Chake, Wesha, Chanja Mjawiri, Pujini, Ukutini, Mtambile, Mkoani na Micheweni.
Alisema alama za mitihani hiyo iligawika katika makundi mbali mbali, ambapo wanafunzi 67 walipata alama A, 120 walipata alama B+, 436 walipata alama B na wanafunzi 418 walipata alama C, huku baadhi ya wanafunzi wakifutia matokeo yao kutokana na sababu za kutokuwa waaminifu wakati wa kufanya mitihani hiyo.
Akizungumza na walimu hao mara baada ya kumalizika kwa mshindano yahoo, mkagunzi wa Elimu kutoa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Pemba, Mwalimu Amour Rashid Aliy, aliwataka walimu hao kuitumia vyema taaluma hiyo waliyopatiwa kwa kwenda kwuafundisha wanafunzi wao.
Alisema mwanafunzi mzuria anayehifadhi Qur-an na kuijuwa ipasavyo lugha ya Kiarabu, basi mwanafunzi huyo hufanya vyema hata katika masomo yake ya skuli za kawaida.
“Mwanafunzi anayehifadhi Qur-an hanatatizo katika masomo yake mengine, ni mwanafunzi anayekuwa bora zaidi darasani na familia yake”alisema.
Alisema taaluma hiyo walioyoipata ni taaluma adhimu, kwani wako walimu wengi wanaitaka nafasi hiyo, lakini hawakubahatika kuipata.
Hata hivyo aliipongeza taasisi hiyo ya Samail Academy kwa juhudi zao wanazozichukuwa katika kuwafundisha watoto lugha ya Kiarabu, huku akiwataka walimu hao kuwa karibu na watoto mayatima ili kuweza kupata Baraka kutoka kwa mungu.

Aliwataka walimu hao kujitahidi kuisoma kwa bidii lugha hiyo, ili kuweza kuwafundisha wanafunzi wao mambo mbali mbali waweze kukisoma vyema Qur-an.
Comments