Kutokana
na matukio ya kiuhalifu yanayoendelea katika baadhi ya maeneo nchini,
leo August 25 2016 Jeshi la Polisi limepiga marufuku mikutano yote ya
kivyama ndani na nje ili kuzuia machafuko ya amani yanayoendelea
kujitokeza katika kipindi hiki.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es salaam Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania, IGP Ernest Mangu amesema Jeshi la polisi halikuzuia mikutano ya ndani ya siasa kwasababu lilikuwa linaamini ni mikutano iliyokuwa ikizungumzia maendeleo ya wananchi
Amesema Jeshi hilo limebaini
kwamba mikutano hiyo imekuwa ikitumika kuchochea wananchi na
kuwahamasisha kuvunja sheria za nchi na kufanya mapambano na jeshi la
polisi
"Kwasababu hiyo basi,kwa
hali ya kutumia mikutano ya ndani kuchochea watu kuvunja sheria na
kupambana na askari, hivyo basi kuanzia sasa jeshi la polisi nchini
linapiga marufuku mikutano yote ya ndani" amesema IGP Ernest Mangu
chanzo;mpekuziblog.
Comments