Hillary Clinton amekubali rasmi
kuwa mgombezi wa Urais wa Marekani kupitia chama cha Democratic, huku
akisema wakati wa kupambana na mpinzani wake sasa umeanza rasmi.
Alitoa
wito kwa wanachama wote wa Democratic kuungana naye huku akimkebehi
mpinzani wake wa chama cha Republican, Donald Trump, katika madai yake
kuwa ni yeye pekee anayeweza kuyasuluhisha matatizo ya Marekani.
Alisema kuwa Wamarekani hufanya kazi kwa pamoja kyatatua yote yanayonufaisha taifa.
Awali, bintiye Chelsea Clinton alikuwa ametoa hotuba na kumsifu sana
mamake. Alisema ni mwanamke ambaye huwa hasahau anawapigania akina nani.
"Watu huniuliza kila wakati, huwa anawezaje kufanya haya? ... ni kwa sababu huwa hawasahau watu anaowatetea," amesema.
"Najua kwa moyo wangu wote kwamba mamangu atatufanya tujionee fahari."
chanzo;bbc.
Comments