Wananchi wa
shehia ya chachani na maeneojirani katika wilaya ya chake chake wametakiwa
kuchukua tahadhali kwa kuwepo kwa maradhi ya kipindu kipindu.
Tahadhari hiyo
imetolewa na naibu sheha wa shehia ya chachani abrahmani shehe mohd juu ya
kukithiri wa ucha kwa baadhi ya maeneo ndani ya shehia hiyo.
Amesema usafi
wa mazingira mihimu katika kila sehe kwani mvua zinazo endelea kunyesha hivi
sasa zinaweza kusababisha maradhi tofauti tofauti.
Amefahamisha
kua ili kujikinga na maradhi hayo ya kipindu pindu nilazima kila mmoja achukue
hatua ya kudumisha usafi pamoja na kuchemsha maji kabla ya kutumia.
Ameeleza kua maradhi ya kipindu pindu ni maradhi hatari
hivyo kila mmoja wetu achukue jukumu la kudumisha usafi na kufuata miongozo ya
wataalamu wafya.
Aidha ametoa
wito kwa wananchi wote kukimbilia hospitali kwa haraka pindi wanapo gudua
dalili za ugonjwa huo.
![]() |
samahani mpenzi msomaji picha hii sio rasmi. |
Comments