Na Hamad Khatib - Micheweni.
Wakulima wa zao la mwani Kisiwani Pemba wamelalamikia juu ya kushuka kwa bei ya zao hilo kutoka shilling 700 Hadi
sh/300 jambo ambalo linarudish nyuma maendeleo yao.
Wakizungumza na Nocomped Community Media wakulima haoa wamesema bei hiyo ni ndogo na haikidhi mahitaji yao kutokana na ugumu wa
kazi wanayoipata ya uzalishaji wa zao hilo.
Bi Kaije Bakari Mbwana na Sharif Shoka Ismail wote wakaazi wa Wilya
ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba wamesema kuwa kazi ya kilimo cha mwani ni
kazi mzito, ambacho wakulima wanatumia nguvu nyingi, pamoja na pesa nyingi kwa ajili ya kutafuta vifaa vya kuendeshea
shughuli za kilimo hicho.
“Tunatumia nguvu, pesa zetu, na hata akilipia lakini kila siku
zikisonga mbele na bei ina pungua mwanzo tukiuza shilling 700 lakin sasa ni 300 ni hali
yakushangaza kwakweli”.
Hatahivyo wakulima hao wamesema kua hawajajua sababu ya kushuka kwa
zao hilo kwani mashamba yao kwa sasa wameimarika na kustawi.

Sambambanahayo wameiyomba serikali na makampun ya ununuz wa zao
hilo kuwaongezea bei ili kuweza kujiendeleza kimaisha pamoja na kuondokana na
halingumu ya kimaisha.
Comments