Tahadhari yatolewa juu ya kipindu pindu Micheweni Pemba.

baadhi ya akina mama wakiskiliza ushauri wa dr Fatma.
Wananchi wa kijiji cha Kiuyu Mbuyun Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba wameshauriwa kutumia maji yaliyowekewa dawa kwa ajili ya kuzuia maambukizo ya maradhi ya kipindu pindu.
Wito huo umetolewa na daktar wa hospital ya kiuyu Mbuyun Fatma Juma Hariri wakati akizungumza na wananchi hao juu ya njia za kujikinga na maradhi ya kipipndu pindu ambacho kimekua tishio kwa  wakaazi wa kijiji hicho na hata taifa kwa ujumla.
Amesema lazima tuelewe  kuwa maradhi ya kipindu pindu ni maradhi ambayo yanasambaa zaid katika kipindi kama hichi cha mvua, hivyo ni kufuata miongozo ya madaktar ili kuweza kunusuru familia zeo  na majanga kama hay.
“Ndungu wananchi lazima tuelewe kua kipindu pindu ni maradhi hatari ambayo yanaweza kutuhatarishia maisha yetu hivyo hatuna budi tujikinge nayo ili tuweze kunusuru maisha yetu.
Amesema ili kujiepusha na maradhi ya kipindu pindu nilazima jamii kudumisha usafi wa mazingira katika maeneo yao yanayo wazunguka na kuchukua hatua za haraka pindi wanapo hisi mmoja wao anaugua maradhi kama hayo kumuwahisha hospitali kwa ajili kupatiwa matibabu.
mama akichemsha maji.
Sambamba nahayo amewataka wananchi hao tumia maji ya kuchemsha kabla ya kunwa nay ale yalio wekewa dawa ili kuuwa vimelea vya maradhi vilivyo ndani ya maji hayo.
Kwa upande wao  wananchi wa kijiji cha Kiuyu Mbuyuni  wameahidi kutumia vyema wito huo wa madaktar ili kuweza kunusuru vifo visivyo vitokanavyo na maradhi hayo.
“ tume furahi sana kupata ushauri kama huu kutoka kwa wataalamu sisi tulikua hatujui chochote juu ya kujikinga na majanga kama haya pindi yakitokezea tunawashuku na mungu atawalipa”
Wameeleza kua ujio wa ujumbe huo wa madaktari umekuja muda muafaka kwani utaweza kuwasaidia katika maisha yao ya sasa na yabaadae.



Comments