Zanzibar
Kufuatia matukiombalimbili ya uvunjifu wa amani nchini chama
cha wananchi CUF kimetoa tamko juu ya hali hiyo.
Tamako hilo tolewa leo
na kaimu mkurugenzi wa habari,
uenezi na mawasiliano ya umma Hamad Masoud
Hamad ambapo amesema Tangu kumalizika kwa uchaguzi mkuu wa tareh 25 Oktoba
2015, usalama wa raia wa Zanzibar na mali zao umekuwa katika hali tete.
Taarifa hiyo imesema hali hiyo inatokana na kushuhudiwa kushamiri kwa matukio
ya kuogopesha wananchi na kufurutu ada ukiukwaji wa HAKI ZA BINAADAMU miongoni
mwa wananchi kunakofanywa na vyombo vilivyopewa dhamana ya kuhakikisha ulinzi
na usalama wa nchi na raia wake na mali zao.
Imesema katika siku za hivi kadribuni, hususan baada ya
Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC), Jecha Sali Jecha, kutangaza
kinyume na katiba ya nchi, kufuta uchaguzi wa 25 Oktoba 2015 na matokeo yake,
Zanzibar imeshuhudia uingizwaji mkubwa wa askari, vifaa na zana nzito za kivita
katika visiwa vya Unguja na Pemba.
Sambamba na hayo taarifa hiyo imesema kumekuwepo kwa askari
wengi wa JWTZ wanaorandaranda mitaani wakiwa na silaha nzito za kivita na
operasheni isiyo rasmi ya kuwakamata na kuwabambikizia kesi wananchi wasio na
hatia na hatimaye kuwaweka katika vituo mbali mbali vya polisi na kuwanyima
dhamana hata kwa makosa ambayo kisheria yanapaswa kudhaminiwa.
Taarifa hiyo imesema CUF inaamini pasipo na shaka yeyote kwamba
matukio ya kuchomwa moto kwa masikani na matawi ya CCM huko Pemba ama baadhi ya
nyumba za watu binafsi na mali za serikali ni mambo ya kupangwa dhidi wananchi wasio na hatia.
Katika taarifa hiyo CUF imesema vyombo vya ulinzi na usalama wa nchi vinatakiwa
kakataa kuingia katika mtego wa mipango miovu ya wanasiasa wenye lengo la
kuleta taharuki miongoni mwa wananchi na kuamsha hamasa na kupandisha jazba
zitakazopelekea kuchafuka kwa hali ya amani ya nchi yetu.
Comments