PEMBA
Mkuu wa wilaya ya micheweni Abeid Juma Ali amewataka viongozi
wa dini katika wilaya hiyo kutokubali nyumba za ibada kutumika kwa masuala la
uvunjaji wa amani.
Amesema kuwa kila kiongozi wa dini anapaswa kusimamia na
kushajihisha amani na utulivu na kuwataka wafuasi wao kuwa chanzo cha kuienzi
amani iliyopo hapa nchini.
Kauli hiyo ameitoa wakati akifungua mkutano wa baraza la kusimamia amani , uliofanyika katika ukumbi wa kituo cha
redio jamii micheweni , uliolenga
kuienzi amani pamoja na kuilinda wakati huu wa kuelekea uchaguzi mkuu.
Mkuu huyo wa wilaya ametumia fursa hiyo kuwaasa viongozi hao wa dini kuhakikisha kwamba wanatumia uwezo kuzungumza na wafuasi wao ,
kujiepusha na vitendo vinavyoashiria kuwepo na uvunjifu wa amani .
Nao wajumbe wa baraza hilo wameahidi kuufikisha ujumbe kwa
wafuasi wao ili wasiwe chanzo cha
kuvunja amani na utulivu.
Aidha wameviomba vyombo vya ulinzi kutekeleza wajibu wao kwa
kufuata sheria na taratibu wakati
wanapotekeleza wajibu wao ili kusiwepo na vitisho kwa wananchi.
Comments