Pemba.
JESHI
la Polisi limeanza msako wa watu waliochoma nyumba tano za wananchi wakazi wa
Kangagani, ofisi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Kituo cha Afya katika Mkoa wa
Kaskazini Pemba.
Akizungumza
na mwandishi wa habari hizi kwa njia ya simu , Kamanda wa Polisi Mkoa wa
Kaskazini Pemba, Hassan Nasiri Ali, alisema katika matukio hayo hadi sasa
hakuna mtu anayeshikiliwa Polisi wala hakuna aliyejeruhiwa na Jeshi la Polisi
linaendelea na uchunguzi kuhusu matukio hayo.
Awali
Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba, Omar Khamis Othman alipiga marufuku
mikusanyiko ya watu katika nyakati za usiku ikiwa ni sehemu ya kujaribu
kupambana na kupunguza vitendo vya hujuma alivyosema vimelenga kuvuruga
uchaguzi wa marudio unaotazamiwa kufanyika Machi 20 mwaka huu.
Naibu
Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Vuai Ali Vuai alisema matukio hayo yamelenga
kuhujumu na kutisha wananchi ambao ni wafuasi wa chama hicho, ili wasijitokeze
kupiga kura katika uchaguzi wa marudio.
Vuai
aliwataka wafuasi wa CCM kuwa watulivu katika kipindi hichi kigumu na kuviachia
vyombo vya dola kufanya kazi yake ya uchunguzi na kuwatia hatiani watuhumiwa wa
matukio ya hujuma, ambayo hivi sasa yamekuwa yakijitokeza kwa wingi Pemba .
Comments