NOCOMPED COMMUNITY MEDIA

Zanzibar
Jeshi la Polisi Zanzibar limewakamata watu 20 kwa tuhuma za kuchoma moto Nyumba,  matawi ya CCM na majengo ya huduma za jamii pamoja na waliomzomea Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein, kisiwani Pemba.
Watu hao wamekamatwa kutokana na msako mkali unaoendelea  katika mikoa miwili visiwani humo tangu miundombinu hiyo,  kuhujumiwa kwa kuchomwa moto kwa sababu zinazodaiwa kuwa  za kisiasa.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa Kaskazini Pemba, Hassan Nassir, alisema jana kuwa watu 20 wamekamatwa kwa tuhuma za kuhusika na matukio uchomaji moto majengo.
Alisema pamoja na kukamatwa kwa watu hao, polisi wanaendelea kuimarisha ulinzi wa doria wa kuwasaka watu wengine na kuchunguza chanzo cha hujuma hizo.
Matukio ya kuchomwa moto nyumba, matawi ya CCM na majengo ya huduma za jamii, yametokea huku Rais wa Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein, akiendelea na ziara ya kikazi kisiwani Pemba.

Majengo yaliyochomwa moto yamefikia 15, zikiwamo Ofisi za CCM katika matawi ya  Tibrinzi, Kipapo, Shidi Mkanyageni, Muambe na Kendwa.

Comments