Pemba
Kutokuwepo kwa usafiri wa uhakika, kwa walimu wanaosomesha skuli ya kisiwa cha
Kokota shehiya ya Mtambwe wilaya ya Wete Mkoa wa kaskazini Pemba, ni miongoni
mwa changamoto kubwa inayo wakabili walimu hao wakati wanapokwenda kusomesha.
Walimu hao ambao wanatumia vyombo kama mashua na ngalawa za wavuvi
wakati wanapokwenda kisiwani humo, imekuwa ikiwawiya vigumu kufika na kuondoka
kwa wakati, licha kutumia shilingi 3000 kwa kila siku.
Akizungumza na mwaandishi wa habari mwalimu mkuu wa skuli
hiyo ambae ni ni muathirika wa tataizo hilo,
Juma Ali Hamad alisema usafiri huo ambao walimu wanatumia vyombo hivyo
hulazimika kukaa humo baharini kilomita 25 hadi kufika kisiwa hicho.
Alisema kuwa kutokana na kutokuwa na uhakika wa usafiri,
husababisha wakati mwengine kuchelewa kuwapatia watoto haki yao ya elimu, jambo
ambalo linavuru mpangilio mzima w avipindi.
Baadhi ya wanafunzi wanaosoma skuli hiyo, wamelalamikia
uchelewaji wa waalimu wao kutokana na kukosa usafiri wa uhakika, hali ambayo
huwakosesha mpangilio madhubuti wa usomeshwaji.
Mratibu wa Idara ya elimu
ya Maandalizi na Msingi Pemba Faki Sleyyum Faki alisema kuwa, katika
suala hilo la usafiri kwa waalimu hao, awali walikuwa wakilipwa shilingi 60,000
na kuongezewa hadi kufika 100,000 kwa lengo la kufidia nauli.
Skuli ya kisiwa cha Kokota ambayo inawaalimu watano ambao
wote wanaishi nje ya kisiwa hicho, akiwemo Mwalimu mkuu, na hulazimka kila siku
kutumia usafiri wa kujitegemea wa mashuwa kwenda skulini humo.
Comments