NOCOMPED COMMUNITY MEDIA

Pemba
Manahodha wa Vyombo vinavyovuusha wananchi kutoka Kisiwa Panza kwenda Chokocho, wamatakiwa kuacha tabia ya kugoma kuwavuusha wananchi kwa madai ya itikadi za kisiasa.
Hali hiyo imekuja hivi karibuni maeneo hayo kua baadhi ya wanachi  wamemadai kugomewa na kutokuvuushwa kutoka kisiwa hicho Kwenda Chochoko, hali inayowapa shida wananchi wanaoishi katika maeneo hayo.
Akizungumza wananchi wa kisiwa Panza Wilaya ya Mkoani Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa kusini Pemba, Mhe: Mwanajuma Majid Abdalla alisema chombo chochote kitakacho goma kuwavusha wananchi kitachukuliwa hatua kali za kisheria ikiwemo kukipandisha juu hadi kuozeana na hodha wake atafikishwa kwenye vyombo vya sheria, akisema kuwa kufanya hivyo ni kuwanyima wananchi uhuru wao.
Mh:Mwanajuma ameitaka Mamlaka ya usafiri baharini kuhakikisha inavifutia usajili vyombo vyote vitakavyo goma kuwavusha wananchi katika kisiwa Hicho.
Mkuu huyo wa Mkoa aliwataka wananchi kuhakikisha wanaendelea kudumisha amani na Utulivu uliyopo nchini, kwani wananchi wote wa kisiwa Panza ni ndugu.
Kwa upande wake Kamanda wa Polisi Mkoa wa kusini Pemba, Sheikhan Mohamed Sheikhan, alisema eneo la usafiri ni huru hivyo picha, rangi na bendera zote zilizopo zinapaswa kupachuliwa, kwani maeneo huru hayana itikadi ya vyama vyovyote vya siasa.

Kwa upande wao wananchi wa Kisiwa Panza, waliwataka manahodha kuacha tabia ya kuwagomea kuwavuusha kwa itikadi za kisiasa kwani kufanya hivyo ni kukiweka pabaya kisiwa Chao.

Comments