NOCOMPED COMMUNITY MEDIA

''Vyombo vya habari vinachochea Z'bar''

Na Muhamed Khamis, Univeristy Of Iringa


Sikutaka kuamini kirahisi lakini baada ya kuona mifano kadhaa ilinibidi niamini na kuhisi tulichofundishwa kilikuwa na ukweli ndani yake.

Tukiwa wanafunzi wa Chuo kikuu Iringa, mkufunzi wetu wa somo la Photojournalism alituambia na kutuelekeza kuwa vyombo va habari vya magharibi vinaichafua Africa na kuionesha kwa ubaya ukilinganisha na matokeo mbali mbali ya bara la ulaya.

Nakumbuka mkufunzi huyu (Mr.Aloyce) alitoa mfano tukio la September 11 Nchini Marekani baada ya kubomolewa majengo kadhaa kufuatia mashambulizi ya ndege. 

Katika tukio lile hakuna chombo chochote kilichowahi kuonesha picha jinsi watu walivouwawa au kuonekana kwa damu yoyote hile.

Alituambia kila kitu kilifichwa ili watu wasielewe ukweli na huu ndio mfumo wanaoutumia vyombo vya habari ya magharibi kuzilinda nchi zao.

Alitutaka kuvuta kumbukumbu ili tukumbuke tokeo la Westgate Nairobi Kenya au hata lile la Garissa jinsi tv hizi za magharibi zilivoonesha mtapakao wa damu kila sehemu bila hata kuficha kitu kiasi ambacho nathubutu kusema walikwepa kabisa maadili na miiko ya taaluma zao.

Ingawa upo utafauti lakini kwa kiasi kikubwa haitofautiani sana na kwetu,kama hujawahi kufika Zanzibar na umebahatika kusoma magazeti unaweza kudhani ni kesho tu vita vinaweza kutokea Z’bar lakini wapi hali haipo hivyo.
chanzo;http://www.zanzinews.com/

Comments