
Mwakilishi wa Russsia katika taasisi za kimataifa zenye makao mjini
Vienna nchini Austria amesema kuwa jumbe za Iran, China na Russia
zimejadiliana huko Vienna kuhusu hatua mazungumzo yajayo ya JCPOA.
Mikhail Ulyanov ameeleza kuwa, wajumbe za nchi tatu za Jamhuri ya
Kiislamu ya Iran, China na Russia jana Jumatatu walifanya kikao huko
Vienna ambapo walijadili hali ya mambo ya sasa na njia za kuhuisha
mapatano ya JCPOA.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo, ujumbe wa Iran katika kikao hicho cha
pande tatu ulieleza mitazamo na maoni yake kuhusu matini ya rasimu na
masuala yaliyosalia katika mazungumzo ya Vienna. Wakati huo huo wajumbe
za China na Russia pia waliwasilisha baadhi ya maoni na mapendekezo yao
na kusisitiza tena kuwa nchi zao zinaunga mkono kikamilifu misimamo ya
Iran.
Jumbe zote tatu za Jamhuri ya Kiislamu
ya Iran, China na Russia pia zimesisitiza kuwa zinaunga mkono
kuendelezwa kazi kwa jadi bila ya kuharakisha wala kuchelewesha.
Duru ya tano ya mazungumzo ya JCPOA
ilianza Jumanne wiki iliyopita ikihudhuriwa na wawakilishi wa kundi la
4+1 huko Vienna, Austria.
parstoday.
Comments