Waandishi wa habari watakiwa kuandika mwendelezo wa kesi za Udhalilishaji.


Image result for waandishi wa habariWaandishi wa habari kisiwani Pemba wametakiwa kuandika na kuzifuatilia kwa kuzifanyia muendelezo  habari za udhalilishaji kutoka mahakamani kwa kufuata miongozo na maadili ya habari.

Ushauri huo umetolewa na Afisa mradi wa kupinga udhalilishaji Asha Abdallah Makame wakati wa mafunzo maalum kwa waandishi wa habri ya kuwajengea uwezo wa kuandika habari kutoka mahakamani yaliyofanyika katika ofisi za Tamwa chake chake Pemba .

Bi Asha amesema waandishi wengi  baada ya kuandika hawazifanyii mwendelezo habari zao hivyo amewataka kuzifuatilia kwa kina   ili kuwajuilisha wananchi namna ya   kesi zinavyoendelea .

"Waandishi walio wengi huwa wanaandika habari za udhalilishaji  lakinhi shida inakuja baada ya kufika mahakamanhi watu wanasubiri kujua kesi inaendeleajae unakuta mwenhdelezo wake haupo,niwatake waandishi munapoandika habari basi zufuatilieni mpaka hukumu itoke hapo itakuwa umeiridhisha jamii".amesema Asha.

Akitoa mafunzo hayo wakili wa serekali  kutoka ofisi ya mkurugenzi wa mashtaka Juma Ali Juma amesema waandishi wana dhima kubwa ya kuhabarisha jamii  juu ya mwenendo wa kesi za udhalilishaji zinavyoendelea mahakamani .

"waandishi muna dhima kubwa, jamii inategemea kutoka kwenu kusikia namna gani kesi zinavyoendelea pamoja na hukumu zinazotolewa"amesema wakili Juma.

Kwa upande wao baadhi ya waandishi wamesema uwepo wa urasimu mkubwa juu ya upatikanaji wa taarifa kutoka mahakanhi nhdio sabgabgu iliyopelekea kuwawia vigumu kupata muendelezo wa habari zao wanazozitoa.

"Kiukweli upatikanaji taarifa jinsi kesi zinavyoendelea inakuwa shida sana unafika kwa wahusika kutaka kupata taarifa juu ya muendelezo wa kesi kila mmoja anamtupia mpira mwenzake mara nenda kwa msemaji Wete, wakati mwengine wanasema wao hawajapata ruhusa ya kuzungumza alimradi inakuwa shida mpaka unaamua kuachana nayo kwa usumbufu unaoupata". wamesema waandishi.

Comments