
Waziri
wa Kilimo Maliasili mifugo na uvuvi zanzibar, Mh. Mmanga Mjengo Mjawiri,
amesema hataweza kumnyamazia mtumishi yoyote wa wizara yake alieshiriki
kudhorotesha shughuli za miradi katika kuwasaidia wananchi.
Mh.
Mmanga ameyasema hayo huko katika bonde la umwagiliaji machigini, wilaya ya
mkoani, mkoa wa kusini pemba.
Amesema
kuwa, kuna baadhi ya watendaji wamekuwa wakisimamia miradi yao kipindi cha
mwisho cha mkataba kwa malengo ya kufanya ubabaifu huku huduma zikisuasua bila
maelezo yamsingi.
Amesema,
kwa sasa wananchi wamehamasika kuendeleza shughuli za kilimo hakuna haja ya
kuwasumbua na kuwapa sababu zisizo na msingi na kufanya ujanja na badala yake
kuwapatia teknolojia za kutosha kulingana wakati ,ili waweze kupata tija.
Akitoa
taarifa ya utekelezaji wa shughuli za mradi wa kuongeza tija kwa wakulima
(ERPP) katika bonde la machigini afisa mkuu idara ya umwagiliaji, Mbarouk Ali Mgau,
amesema ni kipindi cha miezi sasa tokea kukamilisha malipo kwa shirika la umeme
lakini bado hawajapatiwa huduma, hali inayodhorotesha shughuli za wakulima wa bonde hilo.
Kwa
upande wao wakulima wa bonde hilo, wamesema kuwa, kwa muda mrefu wamekuwa
wakikabiliwa na tatizo la umeme ambao ungaliwasaidia katika kuvutia maji ndani
ya bonde lao pamoja na ubovu wa miundombinu ya umwagiliaji.
Comments