Serikali
imewataka wananchi kuacha kujenga nyumba au kupanda miti ya kudumu katika
maeneo ambayo yametengwa kwa uwekezaji.
Kauli
hiyo imetolewa kwa nyakati tofauti huko CHAMANANGWE na MICHEWENI na waziri wa
ardhi nyumba maji na nishati Salama Aboud Talib chini ya jopo la mawaziri wanne
waliotumwa na Serikali kushughulikia mizozo ya wananchi waliojenga na kupanda miti
ya kudumu katika maeneo ya uwekezaji.
Mheshimiwa
Salama amesema ifikie wakati wananchi kutambua kwamba maeneo ya uwekezaji
hayaruhusiwi kufanyiwa kitu chochote mbadala ya kilichoelekezwa na Serikali hivyo
si busara kwa mtu kujichukulia eneo bila ruhusa kutoka mamalaka husika.
Awali
sheha wa Shehia ya Kiuyu Minungwini Yahya Salim Amir ambaye eneo lake la
Chamanangwe linalomilikiwa na wizara ya kilimo limejengwa nyumba tano na
kutumika kwa kilimo amewashauri wananchi kukubali kufanyiwa tathmini ya mali
zao na kuhama ili kuiwachia Serikali kufanya shughuli zake.
Naye
Mkuu wa Wilaya ya Micheweni Salama Mbarouk Khatib amesema watahakikisha kuona
maeneo hayo yaliyotengwa hayatumiwi
vibaya .
Comments