Mkuu wa Mkoa wa
Kaskazini Pemba Mh.Omar Khamis Othman ,ameipongeza timu ya tano ya madaktari wa
Kichina kwa kwazi nzuri wanaoifanya huko maabara ya kichocho mkoroshoni
kwa kuendelea kutoa huduma za matibabu Kisiwani Pemba kwa wagonjwa
wanaosumbuliwa na ugonjwa huo ambao unaendelea kuathiri wananchi .
Kauli hiyo ameitoa huko Maabara ya kichocho
Mkoroshoni wakati alipokuwa akizungumza na viongozi wa serikali kutoka Wizara
mbali mbali za Pemba kwa lengo la kujua maendeleo ya mradi huu wa kutibu kichocho
unaofadhiliwa na serikali ya kichina ili kuweza kutoa ushirikiano katika
utendaji wa kazi kwenye shehia
zilizoingia kwenye mradi huo.
Mkuu huyo wa Mkoa alisema kazi kubwa iliyombeleyao
nikuwahamasisha wananchi kuata maelekezo yanayotolewa na watalamu hao kuona
ugonjwa huo unaondoka kwa wananchi unguja na Pemba .
Hata hivyo alimtaka kiongozi wa timu hiyo kumuomba
balozi wao wa China aliyepo Zanzibar kumuomba Rais kuwatembelea kuangalia kazi
wanazonzifanya na hatua waliofikia kwa utoaji wa matibabu ya ugonjwa huo.
Nae Mkuu wa kitengo
cha kichocho Pemba Saleh Juma Muhammed, alisema lengo la Mradi huo nikuondosha
Ugonjwa huo na kwa hatua ya kwanza ni kuwauwa konokono kwa kuwatia dawa mitoni
ambako ndio kwenye mazalia yao.
Alifahamisha kwamba
waliamua kulifanyia kazi eneo la Uwandani kwa majaribio kwani ndio eneo kubwa
lilokuwa limeathirika hapo awalikuwavasilimia 8.59 kiwangon hicho ni
kikubwa na sasa tumefikia asilimia 0.6 baada ya kuwapima watu zaid ya 100
ambao waligundulika wanaugua kichocho.
“kwa kweli tukipoanza kuingia kijiji cha uwandani
ilikuwa hali ni mbaya lakini kwa mashirikiano ya wananchi viongozi wa shehia
tumefanikiwa na lengo tumefikia” alisema.
Aidha alifahamisha kwamba baada ya kupatamafanikio
kijiji cha Uwandani ambako tuliweka kama majaribio kuna vijiji vyengine nako
tunatoa matibabu amboko ni Mtangani,na Wingi huko kuna tatizo la ugonjwa
huo.
Kwa upande wake kiongozi wa timu ya madaktari hao
Dr, LUANG YUZHENG, alisema serikali ya China kwa kuendelea kwa mara
nyengine ya mradi wao kwa kuwasaidia wananchi wa Pemba na Unguja kwani ugonjwa
huo umekuwa ukiathiri ugonjwa huo.
Alifahamisha Ugonjwa huo huambukizwa na Konokono
ambae huzaa vimelea milioni moja kwa wakati mmoja kwenye mto kusema
idadi hiyo ni kubwa ambapo isipochukuliwa hatua wananchi
wataendelea kuathirika.
Alifahamisha kwamba matarajio nikupata mafanikio
kulitokomeza gonjwa hilo kama walivyofanikiwa katika nchi yao kwani wananchi
wengi nako wanaathirika kwa matumizi mabaya ya maji katika mito .
Kwa Upande wake afisa Mdhamini wa Wizara ya afya
Pemba Shadya Shaaban Seif, alisema Wizara yake imekua ikitoa mashirikiano
makubwa na madaktar hao pamoja wakuu wa kitengo cha kumbambana na ugonjwa
huo .
Hata hivyo alifahamishakwamba wataendelea
kuwaelimisha wananchi juu athari ya ugonjwa pamoja na kutia dawa kwenye
maziwa.
Afisa Elimu Mkoa Kusini Pemba Mwalimu haji Kombo, alisema
baada ya kuona kazi zinazofanywa na madaktari hao maabara ya Kichocho
atawahamasisha walimu wezake kuelezea athari za ugonjwa wa kichocho kwani kuna
masomo maalumu wanayosomesha katika skuli zao na kusema watapata fursa ya
kuwapeleka wanafunzi hao kusoma na kujua zaidi ugonjwa huo .
Nae Mkuu wa Wilaya ya Chake Chake Rashid Hadidi
Rashid, alisema ataendelea kuzungumza na masheha wake kwenye mikutano yao ili
kuweza kuelimisha jamii ndani ya shehia zao wananchi kuchukua tahadhari ya
kujikinga na ugonjwa huo na kuacha matumizi ya maji kwenye mito na kutunza
mazingira hatarishi ambayo yanachangia maambukizi .
Comments