Kamati ya Baraza la Wawakilishi latembelea kituo cha damu salama Wete Pemba.


KAMATI ya Baraza La Wawakilishi ya Ustawi wa Jamii imetembelea kituo cha damu salama kilichop Wete katika Wizara ya afya Pemba kuangalia shughuli za maendeleo kwa kituo hicho  na utoaji wa huduma   kwa wananchi pamoja na kujua changamoto zinazowakabili watendaji hao.

Akizungumza na wajumbe wa kamati hiyo na viongozi wa wizara ya afya huko ofisi kuu ya Wizara  Wete Pemba Makamo mwenyekiti wa kamati hiyo  Nassor Salum Ali, ambaepia ni mwakilishi wa Jimbo la Kikwajuni ,amesema suala la uchangiaji wa damu salama ni muhimu sana na kusema ameridhishwa na juhudi zinazochukuliwa na watendaji wa wizara na kusema changamoto watazifanyia kazi  zinazowakabili kituoni hapo.

Amefahamisha kuwa rais wa Zanzibar dr.Ali Muhammed Shein, amekuwa akifanya kazi vizur na kuiyunga mkono Wizara ya afya kwa kuboresha huduma muhimu kwa lengo la kuwaondoshea usumbufu wananchi wake.

Nae Mjumbe wa kamati hiyoYussuf Hassan Iddi,ambae pia ni Mwakilishi wa Jimbo la Fuoni amewaomba viongozi na wafanyakazi wa wizara hiyo pemba kufanyakazi kwa mashirikiano  ili kuona mafanikio yanaimarika zaidi  kwa utoaji wa huduma zilo bora .

Kwa upande  wake afisa Mdhamini wa Wizara ya afya Pemba Shadya Shaaban Seif ,  ameishukuru kamati baraza la Wawakilishi ya Ustawi wa Jamii kwa kuwaunga mkono na kusema imesaidia kuwatatulia changamoto tangu kuanza kutembelea  mara kwa mara kisiwani pemba.

Akitoa maelezo kuhusu uwendeshaji wa kituo hicho Mkuu  wa kitengo cha Damu salama Pemba ,Abdi  Kassim Hamadi, amesema licha ya mafanikio makubwa waliyopta tangu kuanzisha kituo hicho pemba wanakabiliwa na changamoto ya kifaa cha utoaji wa majibu ya damu baada ya uchangiaji na kulazimika kuzipeleka Ofisi kuu Unguja iliyopo Amani kwa uchunguzi na kutolewa majibu ya damu hizo nakuwaomba kupatiwa japo mashine ndogo itakayoweza kutoa majibu kwa haraka.

Comments