Wafanyakazi wa sekta zilizogatuliwa waipa ushauri Serekali.


Image result for haji omar kheri
Wafanyakazi wa sekta zilizogatuliwa Mkoa wa Kusini Pemba wameimuomba serikali kuwaongezea wahudumu  na vitendea kazi ili kufanikisha majukumu yao kwa ufanii zaidi.

Wamesema sekta hizo zimekuwa na changamoto ya kiutendaji ikiwemo uchache wa wafanyakzi na wengine kufikia umri wa kustaafu.

Hayo wameyasema kwa nyakati tofauti mbele ya Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ Mheshimiwa Haji Omar Kheir kwenye mikutano ya kusikiliza matatizo yanayozikabili sekta zilizogatuliwa  Kisiwani Pemba.

Wamesema katika kuona maendeleo yanazidi kuimarika ni vyema kwa serikali kubuni nafasi zaidi za ajira na kuzitafutia ufumbuzi  changamoto ndogo ndogo zilizopo.

Katika ziara hiyo waziri afisi ya rais tawala za mikoa serikali za mitaa na idara maalum za smz Mheshimiwa Haji Omar Kheir amesema kwa kushirikiana na viongozi wengine watakaa kuyafanyia kazi matatizo yaliopo ili kuona sekta hizo zinasonga mbele kama ulivyo mpango wa serikali wa kuwaletea wananchi wake huduma karibu nao .

Amesema katika  kuimarisha dhana ya ugatuzi  serikali imepanga katika  bajeti ya  2019-2020 kujenga madarasa 600 unguja na pemba ili kukidhi haja ya ukosefu wa vyuma vya kusomea.

Mapema mkuu wa mkoa wa kusini pemba mheshimiwa hemed suleiman abdalla amewataka wafanyakazi hao kuzidi kujituma huku serikali ikiendelea kuzitafutia ufumbuzi wa kina changamoto zao.

Comments