
Umoja wa UWT wa Mkoa wa Kaskazini umeamua kutoa
msaada wa mashuka hayo kwa hospitali mbili kwa wodi ya akina mama na watoto kwa
kuona umuhimu mkubwa kutokana na mazingira yao kwani kunahitajika usafi wa mara
kwa mara.
Kauli hiyo ameitoa mara baada ya kumkabidhi Mashuka
hayo afisa mdhamini wa Wizara ya Afya hapo hospitali ya Wete ,alisema
kuwa lengo kuu la kutoa ni kutekeleza ilani ya CCM ya Uchaguzi ya Chama cha
Mapinduzi ya mwaka 2015/2020 katika kuhakikisha wanaboresha huduma ambazo
zimeanishwa kwenye ilani hiyo.
Mbunge huyo alisema kuwa wameona ipo haja kutoa
msaada huo ikiwa ni miongoni mwa shamra shamra za kutimia miaka 42 ya kuzaliwa
kwa Chama Cha Mapinduzi ambapo ndio maana ya kutoa msaada huo .
Aidha ameipongeza Wizara ya afya kwa kuborsha huduma
kwa kujenga vituo vya afya kwa kuwasogezea wananchi wake huduma pamoja na dawa
za mmatibabu bure.
“Kwa kweli serikali yetu imekuwa ikiongeza bajet
kubwa kwa kuhakikisha wanaboresha huduma mbali mbali kwenye Wizara zake ili
kufikia malengo ya ilani yetu ya Uchaguzi”.alisema Mbunge huyo.
Akipokea msaada huo Afisa Mdhamini wa Wizara ya afya
Pemba Shadya Shaaban Seif, amemshukuru Mbunge huyo wa Umoja wa akina mama wa
Mkoa wa Kaskazini kwa uwamuzi wake kwa kutoa mashuka 100 ambayo yatatumika kwa
wodi ya mama na watoto kwa kuonyesha kuwa jali wananchi wake.
Aidha alisema msaada huo umekuja wakat muafaka kwani
hospitali ya Wete imekuwa ikipokea wagonjwa wengi ambaob wanalazwa na
kusema watayatumia kama ilivyo kusudiwa na kuwataka wahisani wengine kusaidia .
Nae mwenywkiti wa Mkoa Kaskazni Pemba Miza Khamis
Haji ,aluwomba uwongozi wa hospital ya Wete na Micheweni kuyatunza mashuka
hayo ilikudumu zaidi pamoja na kuthamini michango ya wafadhili
wanayoitoa.
Kwa upande wake afisa uwendeshaji Tiba wa
Wizara ya afya Pemba Dokta Yussuf Hamad Idi, aliwataka madaktar dhamana
walokabidhiwa mashuka hayo kwa hospitali mbili hizo kuhakikisha
wanayatumia ipasavyo ili malengo ya msaada huo ufanikiwe kwa matumizi
yalokusudiwa.
“Nakuombeni wafanyakazi na madaktar mliokabidhiwa
mashuka hayo yatumike kama ilivyotakiwa nitakapo baini mashuka hayo sito
mfumbia macho muhusika atakae kwenda kinyume na msaada huo hatua za
kisheria zitafata juu yake”. alisema.
Wakitoa neno la shukurani mbele ya Mbunge huyo kwa
niaba ya madtar wafanyakazi wengine wa hospital hizo mbili dokta dhama wa
wete Omar Issa Mgongo , alisema wameupokea msaada huo na kuahidi kutumia kwa
malengo yalokusudiwa.
Comments