Wananchi wa Sizini Pemba wapata faraja kujengewa kituo cha afya.


Image result for ali karumeHatimaye wananchi wa shehiya ya sizini na vijiji vya jirani wameanza kupata huduma ya afya ya mama na mtoto baada ya kufunguliwa jengo la kituo cha afya katika shehia hiyo.

Kituo hicho kinatarajiwa kutoa huduma kwa watu wapatao elfu tano (5000) kimejengwa kwa msaada wa zanzibar milele foundation na kuwa na uwezo wa  kutoa huduma ya kujifungulia akina mama wajawazito.

Akifungua kituo hicho huko Sizini Wilaya ya Micheweni katika shamrashamra za miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar mjumbe wa baraza la mapinduzi na waziri wa vijana utamaduni sanaa na michezo Balozi Ali Karume amewataka wananchi   kukitumia kituo hicho kwa dhamira iliyokusudiwa ikiwemo akinamama kujifungulia ili kuimarisha viwango vya afya yao na  watoto wao.

Amesema katika kuyaenzi na kuyalinda mapinduzi hayo ni lazima kila mmoja kuwajibika kwa nafasi yake  katika kuleta maendeleo ikiwemo kujenga na kuvitumia vituo vya afya ili kuwa na afya bora
Mapema Afisa Miradi wa Zanzibar Milele Foundation Pemba Fatma Khamis Silima  amesema ujenzi  kituo hicho  kilichogharimu shilingi milioni mia nne kimejengwa kwa mahitaji maalum kutokana wananchi wa sizini kuwa na kituo kidogo cha afya  na akina mama kwenda micheweni ambako nimbali kupata huduma ya kujifungulia.

akitoa salamu za wilaya ya micheweni kwa balozi ali karume mkuu wa wilaya hiyo salama mbarouk khatib amesema wilaya  ya micheweni na wananchi wa sizini wamefarajika kwa kukabidhiwa kituo ambapo kitaondoa usumbufu mkubwa wa kufuata matibabu masafa marefu.

Comments