
Mwanakijiji wa shehiya ya Mzuri kilichopo makunduchi Rashid Haroun Rashid (29)
amewaomba wasimamizi wa Mradi wa PAZA kusimamia ujenzi wa skuli ya maandalizi mara baada ya
kukamilika ukarabati wa vyoo vya skuli ya Kusini Unguja.
Ameyasema hayo wakati akizungumza na Muandishi wetu ameeleza
kwamba Mradi wa kukuza uwajibija
Zanzibar (PAZA) umefanikiwa kupunguza matatizo mengi katika wilaya ya kusini
Unguja ikiwemo tatizo utoro na uzalilishaji
kwa wanafunzi, uchakavu wa jengo la skuli pamoja na ukosefu wa maji safi
na salama katika wilaya hiyo.
Hata hivyo amesema hana budi kuushukuru Mradi wa PAZA kwa
kuwaondolea shida ya maji katika eneo hilo kwani wananchi wameridhika kwa
kupata maji safi na salama japokua yanatoka kwa mgao lakini wanaamini mradi
ukiendelea maji yatapatikana yakutosha kwa wananchi wa kusini unguja.
Nae Bi Zawadi Hamdu Vuai (53) mkaazi wa shehia ya Mzuri amesema
katika Mkoa wa Kusini kwa sasa utoro na
vitendo vya udhalilishaji kwa wanafunzi vimeondoka, majengo ya skuli
yameboresha na walimu wameongeza kwa kila skuli ambayo iliyokua na uhaba wa
walimu.
Aidha amesema baada ya mradi wa PAZA kuwahamasisha wananchi
njia za kutatua matatizo yanayowakabili katika maeneo wanayoishi, ambapo
vijana wa shehia ya Mzuri, Nganani na Kajengwa wamechukua
hatua kufuata watoto watoro majumbani mwao na kuwapeleka skuli hali
iyopelekea kupunguza utoro maskulini.
Naye afisa elimu kusini Unguja Haji Mohamed Abdulla akijibu
suali la mwandishi aliyetaka kujua mfumo wa ufundishaji wanafunzi amesema
wataendelea na Uwajibikaji kwa wanafunzi kwa kutoa huduma bora na
kuhakikisha ufundishaji unafanyika kwa kufuata mtaala ulioandaliwa na wizara ya
elimu Zanzibar.
Hivyo amesema ofisini yake itaendelea na utaratibu wa kusimamia
majengo ya skuli kuwa safi na mazima pamoja na kuweka mazingira rafiki kwa wanafunzi
ili kuhakikisha wanafunzi wanasoma katika mazingira bora na salama.
Mradi wa kukuza Uwajibikaji Zanzibar (PAZA) ulianza mwaka jana kwa
lengo la kukuza Uwajibikaji Zanzibar ili kuwahamasisha wananchi njia za kutatua
matizo yanayozunguuka katika jamii na utarajiwa kumalizika mwakani.
Na RAHMA MOH’D
Comments