Naibu Waziri wa wizara hiyo, Mohammed Ahmada Salum, alisema hayo
alipofanya ziara ya kutembelea ujenzi wa madaraja ya Kibondemzungu,
Mwanakwerekwe na mtaro wa Kiembesamaki.
Alisema ili kuhakikisha ujenzi huo unakuwa katika viwango, wanafanya
ziara za mara kwa mara katika maeneo hayo ili kuzungumza na wakandarasi
wanaojenga miundombinu hiyo.
Alisema serikali inafanya kila jitihada kuondosha usumbufu na kuwarahisishia usafiri wananchi.
Alisema kukamilika kwa miundombinu hiyo kutachochea mipango ya serikali katika kutekeleza sera ya ukuaji wa uchumi.
“Ujenzi wa miundombinu hii ni utekelezaji wa ilani ya CCM ya 2015-2020, ambayo Dk. Shein anaisimamia,” alisema.
Alisema kukamilika kwa ujenzi wa madaraja hayo ni chachu ya kuondosha
changamoto zote zilizokuwa zikitokea kipindi cha mvua kwa wananchi
kupoteza maisha na miundombinu ya barabara kuharibika.
Mhandisi Nassor Ramadhan, ambaye ni mkuu wa ujenzi wa madaraja hayo,
alisema ujenzi huo umetekelezwa kwa asilimia 30, hivyo alitumia fursa
hiyo kuiomba jamii kuwa wastahamilivu kwani matarajio yao ndani ya mwezi
wa Machi kazi itakuwa imekamilika.
Daraja la Kibondemzungu linayojengwa na kampuni ya MECCO, unatarajiwa
kukamilika Aprili mwaka huu na utagharimu kiasi ya shilingi bilioni
4.8.
Comments