Alisema katika miaka hii 55 ya mapinduzi ya Zanzibar, wananchi wa
Unguja na Pemba, wamefikiwa na huduma za lazima, ikiwemo matibabu,
huduma ya maji safi na salama, barabara na elimu, yaliotekelezwa kupitia
ilani ya CCM bila ya ubaguzi.
Alisema hayo Mjiweni Kengeja wilaya ya Mkoani Pemba, baada ya
kufungua mradi wa maji safi na salama, ikiwa ni sehemu ya shamra shamra
za miaka 55 ya mapinduzi Zanzibar, ambapo kilele chake kitafanyika Pemba
Januari 12, mwaka huu.
Alisema CCM, sio tu imewafikishia huduma wananchi wote, lakini
imesimamia kwa kiasi kikubwa, umoja, mshikamano, amani na utulivu na
kuwafanya wananchi kuishi kwa upendo.
Alisema mfano wa maendeleo yaliosimamiwa na CCM na hasa baada ya
kufanyika kwa mapinduzi ya Zanzibar, ni ufunguzi wa mradi huo wa maji
safi na salama, ambapo utawanufaisha wananchi wa Mjiweni na vijiji
jirani.
Kuhusu mradi huo wa maji safi na salama, aliwataka wananchi
kuhakikisha wanautunza sambamba na kuchangia huduma za maji kwa wakati,
ili ZAWA iweze kufanya matengenezo inapotokezea hitilafu.
Alisema hakuna mwananchi alie na uwezo wa kulipia huduma ya maji,
elimu wala matibabu ndio sababu serikali ikaamua kuweka huduma hizo bila
ya malipo.
Aidha aliwataka vijana na wazee kuendelea kuyaenzi na kuyalinda
mapinduzi ya Zanzibar kwani yamekuwa ndio dira ya kuwafikishia maendeleo
na upendo wazanzibari.
Alieleza kuwa, kabla ya mapinduzi wananchi waliokuwa
wakijishughulisha na kilimo, walilazimika kulipa kodi za ardhi kwa
watalawala na kubakiwa na kipato kidogo, baada ya mavuno.
“Leo kila mmoja anafanya shughuli zake iwe ni ufugaji, uvuvi au
kilimo bila ya kulipia ardhi na anachokipata ni kwa ajili yake na
familia yake,”alieleza.
Zanzibarleo.
Comments