Mfumko wa bei wapungua.

KASI ya mfumko wa bei wa mwaka ulioishia Disemba 2018, umepungua na kufikia asilimia 3.5 ukilinganisha na asilimia 4.4 iliyokuwepo kwa mwaka ulioishia Novemba 2018.

Mkuu wa Kitengo cha Takwimu za Bei Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali, Khamis Abdul-rahman Msham, alisema, mfumko wa bei za vyakula na vinywaji visivyo na kilevi ulipungua kwa asilimia 2.2 ikilingwanishwa na  asilimia 3.4.

Alisema, faharisi za bei  ziliongezeka na kufikia 108 mwezi Disemba ikilinganishwa na 105.1 zilizorikodiwa Disemba 2017.

Alisema, kiwango cha mwaka cha mfumko wa vyakula ulishuka hadi asilimia 2.3 mwezi Disemba ikilinganishwa na asilimia 3.5 kwa mwaka ulioishia Novemba 2018.

Faharisi za bei za vyakula  ziliongezeka  hadi 106.7 mwezi Disemba  kutoka 104.3 kwa mwezi Disemba 2017.

Mkuu huyo, alisema, kwa upande wa bidhaa zisizokuwa za vyakula,zilishuka hadi asilimia  4.3 ikilinganishwa na 5.2.

Alizitaja bidhaa zilizochangia  kushuka kwa kiwango zilikuwa mchele wa Mbeya (6.5%), sembe (19.5%), unga wa ngano (0.4%), ndizi za mtwike (21.6%), ndizi za mkono mmoja (10.3%) na sukari (4.9%).

Kwa upande wa mfumko wa mwezi, uliongezeka kwa asilimia 0.6 mwezi Disemba ikilinganishwa na asilimia ghasi 0.3 kwa mwezi Novemba 2018.

Alisema, kiwango cha mfumko wa bei cha vyakula na vinywaji visivyo na vilevi kiliongezeka hadi asilimia 3.4 mnamo Novemba 2018 kutoka asilimia 2.6 mwezi Oktoba 2018.

Mfumko wa vyakula na vinywaji visivyo na vilevi uliongezeka hadi 1.6 ikilinganishwa na asilimia ghasi 0.5 ambapo ongezeko hilo la mwezi kulichangiwa na kuongezeka kwa bidhaa kama  mchele wa Mbeya (0.8%) na samaki (11.8%).

Alizitaja bidhaa nyengine ni mafuta ya taa (4.5%), petroli (1.7) na diseli (2.0%).

Mkuu wa Takwimu za Kiuchumi Ofisi ya Mtakwimu Mkuu,  Abdulrauf Ramadhan Abeid, alisema, bado mfumko unaendelea kubakia chini ya tarakimu moja katika nchi za Afrika Mashariki na hivyo kwenda vizuri kiuchumi.

Zanzibarleo. 

Comments