Ndugu
wanahabari nawatumia taarifa hii, kwa nia ya kufikisha kilio cha
wakulima wa korosho kwa *Rais wa Jamhuri ya Muungano Dk,John Pombe
Magufuli* kwasababu ndio zao tegemeo la kiuchumi kwa sasa.
Kama
mnavyojua mkoa wa Mtwara umekuwa ukiongoza kwa kuzalisha korosho nyingi
ikifuatiwa na mkoa wa Lindi,Ruvuma na Pwani pamoja na mikoa mingine
mipya ambayo inaongezeka siku hadi siku.
Mtakumbuka
baada ya mvutano kati ya serikali na wafanya biashara (wanunuzi wa
korosho) baadae serikali iliamua kutangaza kuzinunua korosho zote kwa
Tsh.3,300/-kwa kilo.
Zoezi
hili lilifanyika kwa maamuzi ya haraka kabla ya kupata ushauri wa
kitaalamu lakini pia utafiti wa kina wa namna ya kufanikisha zoezi hili
la ununuzi wa korosho ikiwa ni pamoja na kupata uhakika wa soko la
korosho na taratibu zingine.
Hata hivyo, itakumbukwa wakati huo wanunuzi na makundi yao walishauri namna bora ya kutekeleza maelekezo hayo bila mafanikio.
Wakati
wa kikao cha mashauriano cha Mkoa wa Mtwara (RCC) tulipokea taarifa
kwamba kwa mwaka nchi ina uwezo wa kubangua tani 20,000 tu kati tani
270,000 zinazotarajiwa kukusanywa.
Taarifa
hii inapingana na taarifa ya Waziri wa viwanda kwamba tani 100,000
zitabanguliwa na hivyo serikali sasa inatafuta wadau ili wawezi kununua
ziada ya tani 150,000.
Hivyo
ndugu wanahabari, nawaanfikia leo ili kutoa mrejesho wa yanayoendelea
katika mikoa ya Lindi, Mtwara na Pwani kwa wakulima baada ya kufanya
uchunguzi wangu binafsi kama *Mwakilishi wa Wananchi wa Jimbo la Ndanda*
ambao na wao wako katika Kilio cha kutolipwa.
Ifahamike
kwamba, baadhi ya wakulima wanalipwa, wale wanaizalisha zaidi ya tani
1.5 wao hawalipwi, wakiwemo makundi ya *Wazee, wajane na warithi* Ivi
kuwaongezea uchungu wa maisha kwa kisingizio cha uhakiki,
*Yafuatayo ni matatizo yaliyopo kwenye tasnia ya Korosho kwa sasa*
1. Utaratibu wa malipo umekuwa wa kusuasua sana tofauti na taarifa alizopewa *Mheshimiwa Rais na Waziri Mkuu*
2. Wakati kinachodaiwa kuwa zoezi la *uhakiki* kikiendelea kuna *viashiria vya rushwa* kutoka kwa wahakiki.
3. Wakulima wamegawanywa kwa makundi makundi na hivyo kuwafanya wawe wanyonge zaidi
4.
Taarifa za malipo zimekuwa za siri kiasi kwamba hata viongozi wa vyama
vya msingi hawana taarifa wala kufahamu kinachoendelea juu ya wakulima
waliokusanya korosho maghalani, ivyo kuhatarisha uhai wa vyama ambavyo
vitakumbwa na madeni makubwa, yakiwemo ya wabebaji na wasafirishaji.
5.
Matumizi makubwa ya nguvu kutoka vyombo vya ulinzi na usalama, jambo
hili liko maeneo mengi, kubwa zaidi ni tukio lililotokea Nachingwea,
viongozi wa vyama vya msingi wamepigwa na wanajeshi kwa kushirikiana na
polisi ofisini kwa Katibu tawala (DAS), ushahidi upo na waliofanya tukio
hilo wanafahamika kwa majina
6. Uwezo mdogo wa wahakiki na ujuzi kuhusiana na zao la korosho, wahakiki nao wako mafunzoni, badala ya kutekeleza wajibu
7.
Malalamiko yanayotolewa chinichini kutoka kwa wasimamizi wa zoezi la
uhakiki, kuhusu posho zao na stahiki nyingine, ivyo kuongeza gharama za
uendeshaji, overhead cost
8.Kuna dalili zote za kutokea kwa utaifishaji wa mali za wananchi kwa kisingizio cha kukomesha biashara ya kangomba.
Swali la kujiuliza kama wauzaji wa korosho hizo hawatalipwa na korosho zao zimechukuliwa na serikali, je hii tunaita nini?
Ni kweli kwamba hakuna wachuuzi wa mazao mengine zaidi ya korosho.
Hivyo
ndugu waandishi, kutokana na masuala ya msingi niliyoyataja yanaweza
kuwa na athari kubwa sana kwa mwananchi mmoja mmoja lakini athari kubwa
iko kwa Taifa.
*Naomba niwatajie athari chache zinazoweza kujitokeza sasa hivi na baadae....*
1.
Halmashauri zetu zitashindwa kujiendesha kwa sababu zinategemea kwa
kiasi kikubwa mapato yatokanayo na mazao ikiwemo korosho, mtakumbuka
kwamba mbaazi haikuwa na soko zuri msimu uliopita.
2.
Kuharibika kwa korosho zilizoko maghalani kwa kunyeshewa na mvua, hasa
zile zilizoko mikononi mwa wakulima, na hivyo kupoteza ubora wake ambao
ndio sifa kuu ya korosho ya nchi yetu.
3.
Wakulima kushindwa kujimudu maisha yao ya kawaida mfano kulipia ada za
watoto (private schools) na michango mbalimbali hii pia itasababisha
kushuka kwa elimu, lakini pia wakulima hawa hawa wanashindwa kuandaa
mashamba yao kwa ajili ya msimu ujao, ivyo kupunguza uzalishaji, na
baadae kipato kuendelea kushuka
4.
Kupoteza mapato kwa serikali kwa maana ya *Export Levy na Export
Revenue* hivyo kushusha thamani ya shillingi, na pia kupoteza imani kwa
wafanya biashara wa nnje na wa ndani wa mazao.
5.
Bidhaa kudorora madukani, hasa maduka ya vifaa vya ujenzi na vyakula
kwasababu wafanyabiashara wakishajua ni wakati gani wakulima wanahitaji
biadhaa fulani fulani.
7.Kujengeka kwa chuki kati ya wananchi na serikali hasa kwa wale ambao watadhulumiwa korosho zao.
8.
Kudorora kwa shughuli za maendeleo katika mikoa ya Lindi, Mtwara na
Ruvuma ambao kipindi kama hiki wananchi wanakuwa na kazi nyingi za
maendeleo yao hasa ujenzi na uboreshaji wa makazi, na miundombinu
mingine yakiwemo madarasa zahanati nk
Ni
wakati sasa wa *Mh Rais* kutembelea mikoa ya Kusini na kuwapa wananchi
nafasi ya kuzungumza ili ajionee mwenyewe ni kitu gani kinaendelea kwa
lengo la kumsaidia mkulima na si vinginevyo
Imeandaliwa na;
*Cecil David Mwambe*(Mb)
*Mbunge Jimbo la Ndanda*
Mpekuzi.
Comments