Dongwe walia na tatizo la kuingiliwa na maji.

kwa  tatizo la kuingiliwa na maji taka katika eneo hospital  na skuli ya Bwejuu Dongwe imekuwa ni changamoto kwa wakaazi wa kijiji hicho.

Akizungumza na muandishi wa habari  hizi Chum Haji Ali mwenye umri wa miaka 58 amesema baada kuhamasika kupitia Mradi wa PAZA wameunda kamati yakufuatilia tatizo la maji katika ofisi ya Halmashauri ya wilaya kusini  lakini limeshindikana na maafisa wa maji katika ofisi hiyo wamesema suali la maji watalifuatilia katika ofisi ya mamlaka ya maji Zanzibar (ZAWA) lakini hadi sasa hakuna dalili za upatikanaji wa maji katika eneo hilo.

Akizungumzia kuhusiana na huduma za Afya katika kijijini hapo amesema kwa sasa zimeboresha na kwa upande wa wazazi wamepewa maelekezo endapo watakaopokua tayari kujifungua waelekee spitali ya Jambiani.

Kwa upande wa elimu amesema wanaushukuru mradi wa PAZA kwa kuwafanyia marekebisho Banda moja la Skuli na kuutaka mradi huo kuendelea  kumehamasisha watu kujua utaratibu wa kwenda ofisi ya Halmashauri kufuatilia changamoto zinazowakabili.

Nae Afisa Maji Wilaya ya Kusini Bw Hafidhi Hassan Mwinyi amesema Baadhi ya shehia ya Bwejuu maji yanapatika lakini eneo la Bwejuu Dongwe kuna mwinuko wa ardhi ndio imepelekea waakaazi wa eneo hilo kukosa maji safi na salama .

Hata hivyo ameeleza kwamba hatua za ufumbuzi zinaendelea kushughulikwa hivyo amewaomba wananchi waendelee kustahamili huduma ya maji safi na salama itapatikana .

Kutokana na baadhi ya changamoto walizonazo wanakiji cha Bwejuu Dongwe  hazijatatuliwa  wamekiomba Chama Cha Waandishi wa Habari Zanzibar (TAMWA-ZANZIBAR) kuendeleza maradi wa kukuza Uwajibikaji Zanzibar (PAZA) kutokana na tatizo la maji safi na salama bado halijatatuliwa katika shehia hiyo.

Na RAHMA MOH’D

Comments