Hafla hiyo ilifanyika ikulu mjini Zanzibar na kuhudhuriwa na viongozi
mbali mbali wa vyama vya siasa, serikali, wananchi pamoja na viongozi
wakuu wastaafu akiwemo Rais mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Ali Hassan Mwinyi.
Awali akitoa tamko kuashiria kuanza shughuli hiyo, Katibu Mkuu Ofisi
ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Salum Maulid Salum,
alisema Dk. Shein ametunuku nishani ya mapinduzi 45, nishani ya utumishi
uliotukuka 53 na nishani ya ushujaa 14 kwa viongozi, watumishi wa umma,
maofisa na wapiganaji wa idara za SMZ na wananchi.
Alieleza kuwa sherehe hiyo ilihudhuriwa na watunukiwa 112 ambao kati
ya hao 40 ni marehemu ambao nishani zao zimepokelewa na wawakilishi wao
na 72 wako hai ambapo nishani zao walipokea wenyewe au kupokelewa kwa
niaba yao.
Alisema watunuku wote sifa zao zimekidhi matakwa ya nishani hizo
ambapo nishani ya mapinduzi hutolewa kwa mtu ambaye aliasisi au
alishiriki au aliyatukuza na kuyaenzi mapinduzi ya Zanzibar ya 1964.
Aliongeza kuwa mtunukiwa ni pamoja na kiongozi au mtu mwengine
aliyehai au aliyefariki ambaye aliiletea sifa Zanzibar katika fani mbali
mbali na kuonesha maadili mema ya kusifika na kuigwa ambapo katika
sherehe hizo, nishani ya mapinduzi inatunukiwa katika kundi la viongozi
na wananchi wenye sifa maalum.
Alisema nishani ya utumishi uliotukuka inatolewa kwa mtumishi wa umma
au idara maalum za SMZ aliyehai au aliyefariki ambaye ametimiza
utumishi wake kwa muda wa miaka isiyopungua 20 mfululizo na kwa mtumishi
wa idara za SMZ miaka isiyopungua 20 ya kuwa ofisa na katika kipindi
chote hicho amekuwa na tabia njema.
Aliongeza kuwa mtumishi huyo awe ametumikia taifa kwa uzalendo wa
hali ya juu na kufanya kazi kwa kujitolea, uwajibikaji, uadilifu,
ujasiri na umakini katika kusimamia majukumu na utendaji kazi.
Aidha, alieleza kuwa nishani ya ushujaa inatolewa kwa mtumishi wa
idara maalum za SMZ au mtu mwengine yeyote aliyehai au aliyefariki
ambaye ametenda kitendo cha ushujaa, ujasiri na uzalendo ambacho
kimesaidia kuokoa mali au uhai wa mtu au kujitolea maisha yake kwa ajili
ya ulinzi wa taifa.
Pamoja na hayo, alieleza kuwa vitendo hivyo vya ushujaa viwe wazi
ambavyo alivifanya na kuthibitishwa, mahala popote pale penye hatari na
ameendelea kuwa muaminifu na mtiifu kwa nchi na serikali yake.
Nishani zilizotolewa ni pamoja na nishani ya mapinduzi kwa viongozi
na wananchi wenye sifa mbali mbali akiwemo CP Ali Abdalla Ali, Balozi
Omar Ramadhan Mapuri, Dk. Mohamed Seif Khatib, Said Bakari Jecha na Meja
Mstaafu, Haji Abdalla Sadala.
Wengine ni Balozi Mohamed Mwinyi Mzale, Abdulrahman Mwinyi Jumbe,
Masauni Yussuf Masauni, Abdalla Rashid Abdalla, Msham Abdalla Khamis,
Biubwa Amour Zahor, Joha Shaali Khatib, Sihaba Ismail Faraghani, Said
Rashid Mohamed, Kombo Hassan Juma, Haji wa Haji wa Haji, Mohamed Iddi
Juma, Amina Khamis Borafia.
Dk. Shein pia, aliwatunuku Khatib Idi Khatib, Mohamed Yahya Juma,
Salum Hassan Mzee, Khamis Amour Mzee, Borafia Silima Juma, Kombo Ali
Vuai, Salim Ali Matta, Juma Ali Juma, marehemu Rashid Mohamed Khamis,
marehemu Haji Kombo Mbaraka, marehemu Othaman Bakari Othman na marehemu
Ame Mohamed Juma.
Wengine waliopewa nishani hizo ni marehemu Said Mwinyichande Mkanga,
Safia Maneno Suleiman, marehemu Ali Khamis Suleiman (Ali Kima), marehemu
Juma Othman Faki, marehemu Ramsa Mbarouk Foum, marehemu Hussein Ayoub
Mussa, marehemu Hassan Faki Kombo na marehemu Jafari Ali Haji (Suwedi
Mabugira), marehemu Omar Ussi Muhidini na marehemu Said Mussa Ali.
Aidha, Dk. Shein alitoa nishani ya Mapinduzi kwa timu za mpira na
vikundi vya uhamasishaji vikiwemo timu ya Zanzibar Heroes 2017, timu ya
Zanzibar ya mpira wa ufukweni 2017, bendi ya Safari Trippers na kikundi
cha taarab cha Siti Binti Saad.
Pamoja na hayo, Dk. Shein alitoa nishani ya utumishi uliotukuka kwa
watumishi wa serikali wakiwemo Balozi Hussein Said Khatib, Julius B.
Raphael, Salmin Senga Salmin, Dk. Mohamed Saleh Jidawi, Uledi Mwita
Kisumku, Khadija Ali Mohamed, Ahmed Himid Mbaye, Tamim Amour Hassan na
Said Mohamed Hussein.
Comments