Azam yairambisha Yanga

TIMU ya Azam FC imeendeleza ubabe kwa Yanga SC kwenye michuano ya Kombe la Mapinduzi baada ya kuitandika mabao 3-0 katika mchezo wa Kundi B usiku huu Uwanja wa Amaan, Zanzibar.

Mshambuliaji Mzambia, Obrey Chirwa aliifunga mabao mawili timu yake ya zamani dakika za 33 na 60, wakati bao jingine  lilifungwa na kiungo Mghana, Ennock Atta-Agyei dakika ya 40.

Azam FC inafikisha pointi nne baada ya ushindi huo kufuatia sare ya 1-1 na Jamhuri ya Pemba katika mchezo wa kwanza na kupanda kileleni mwa Kundi B.

Comments