Mazungumzo hayo kati ya Morocco na
harakati ya Polisario kuhusu mzozo wa Sahara Magharibi yalifanyika jana
katika kikao cha faragha kwa kuhudhuriwa na Horst Koehler, Mjumbe wa
Umoja wa Mataifa katika masuala ya eneo la Sahara Magharibi.
Ripoti
zinaonyesha kuwa, mazungumzo ya awali kuhusu mzozo wa Sahara Magharibi
yamekuwa na matokeo ya kuridhisha.
Koehler amesema anataraji kuwa
mazungumzo hayo ambayo yalikwamza tangu mwaka 2012 yatahuishwa upya na
itapatikana njia ya ufumbizi itakayoridhiwa na pande zote mbili husika
ili kuhitimisha mzozo wa Sahara Magharibi.
Harakati ya Polisario imekuwa
ikiiendesha mapambano tangu mwaka 1973 ya kupigania uhuru wa eneo la
Sahara Magharibi kutoka kwa Morocco.
Mapigano kati ya serikali ya
Morocco na harakati ya Polisario yalianza mwaka 1975 na mwaka 1993
kulitiwa saini makubaliano ya kusitisha vita kati ya pande mbili hizo
chini ya usimamizi wa Umoja wa Mataifa.
Serikali ya Morocco inataka kuibakisha
Sahara Magharibi chini ya mamlaka yake na kuipatia mamlaka ya utawala wa
ndani. Hata hivyo harakati Polisario inapinga mpango huo na inatoa wito
wa kuitishwe kura ya maoni kwa ajili ya kuainisha mustakbali wa eneo
hilo.
Comments