Katika baadhi ya vituo kama Chuini, Nyerere, Mtopepo, Haile
Sellasie, Lumumba, Vikokotoni, Kiponda, Jang’ombe Kidongochekundu, na hata kwa upande Pemba imebainika
wanafunzi wakifanya mitihani yao bila bugdha huku ulinzi ukiwa umeimarishwa.
Baadhi ya wasimamizi wa vituo hivyo, ambao hawakutaja majina yao
kutajwa, wamesema mitihani inaendelea vizuri na hakuna matukio mabaya
yaliyoripotiwa.
Wameipongeza serikali kwa kuimarisha ulinzi ili kuhakikisha
hakuna matukio yoyote ya udanganyifu yanayotokea.
Walisema mitinani inafanyika kwa utulivu mkubwa huku wasimamizi
wakitekeleza kwa vitendo kanuni zote za mitihani hiyo.
Aidha ulinzi umeimarishwa katika vituo vya mitihani ikihusisha polisi
pamoja na vyombo vyengine vya ulinzi na usalama nchini.
Kwa siku ya jana watahiniwa walifanya mitihani ya Kiswahili
wakati wa asubuhi na kumaliza na mtihani wa somo la uraia wakati wa jioni.
Watahiniwa laki 427,181 wamesajiliwa kufanya mtihani hiyo ambapo
kati yao watahiniwa wa skuli za serekali ni laki 368,227 na wa kujitegemea ni 58,954.
Comments