SMZ kuendelea kuimarisha huduma za Afya.


Naibu waziri wa afya Zanzibar Mh. Harusi Said Suleiman amesema serekali itaendelea kutekeleza wajibu wake katika kuwafikishia wananchi huduma muhimu kwa kuzingatia mahitaji yanayo hitajika.

Akizungumza na watendaji wa hospitali ya chake chake mara baada ya kuzindua vitengo vitatu ndani ya hospitali hiyo amesema muda umefika sasa kwa wananchi wa Kisiwa cha Pemba na maeneo mengine kuzienzi huduma zinazo tolewa ili kuweza kufikia malengo yalio kusudiwa.

Akizindua kitengo cha viuongo badia Hospitalini hapo Mh. Harusi amesema kitaweza kuondoa changamoto za muda mrefu kwa wananchi wa Pemba ambao walikua wakihitaji huduma hiyo kwa muda mrefu na sasa Serekali kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo wameweza kulitatua kwa haraka.

Amesema kitengo hicho kitaweza kuondoa changamoto ambazo kwa kipindi kirefu wananchi walikua wakikilalamikia nakupunguza ghara kubwa ya kuweza kuitafuta huduma hiyo kwa masafa marefu hivyo nivyema kwa wananchi kuitumia fursa hiyo ili waweze kujikimu katika mahitaji yao kwa muda muafaka.

Amefahamisha kuwa ili kuweza kufikia malengo yaliokusudiwa nivyema kwa madaktari kuvitumia vifaa vilivyo tolewa na kuvithamini pamoja na kuvifanyia matengenezo pale panapo stahiki kwalengo la kuweza kuwahudumia wananchi muda mrefu pasipo kuchakaa haraka.

Wakati huwo huwo amepata fursa ya kufungua kituo cha mkono kwa mkono katika hospitali hiyo nakusema kuwa lengo nikupambana na matukio yote ya udhalilishaji yasizidi kuendelea huku akiwataka watedaji wake kutoa mashirikiano kwa walengwa.

 Hatahivyo ameyashukuru mashirika ya save the chidren pamoja na Infant Club Foot Appeal kwa kuweza kuisaidia hospitali hiyo ambayo nikimbilio la wananchi wengi kisiwani Pemba.

Akitoa neno la shukurani kwa wafadhili walio jitokeza kusaidia vifaa hivyo Afisa madhamini Wizara ya Afya Shadia Shaaban Seif  amesema vimekuja muda muafaka kwani wataweza kuwahudumia wananchi wanao hitaji kupatiwa msaada wa hali hiyo.

 Kwaupande wake mwakilishi wa shirika la Infant Club Foot Appeal lenye makao yake makuu nchini Uiengereza Dr. Shault Houcking amesema wataendelea kuisaidia Zanzibar ili iweze kufikia maendeleo endelevu kwani kila mmoja anawajibu wakufanya hivyo kwa nafasi zao tofauti.

Nae mtaalamu wa viungo badia Dr. Salim Seif Ali amesema wamefarajika kupatiwa vifaa hivyo ambavyo vitaweza kuwasaidia kuweza kutoa huduma zilizobora kwa wananchi pindi wanapo hitaji.

Jumla ya vitengo vitatu vimezinduliwa katika Hospitali ya Chake Chake ikiwa nipamoja na kitengo cha viungo bandi, Kituo cha Mkono kwa mkono na kitengo cha Tv ambacho kitawasaidia wananchi kupata elimu ya afya na mambo mengine.
Mwakilishi wa ICA Dr. Shault Houcking akitoa maelezo kuhusu misaada yao.

Mkuu wa kitengo cha viungo bandia Dr. Salim Seif Ali akielezea jinsi viungo hivyo vinavyo tumika.
Afisa mdhami Afya Shadia Shaaban Seif akitoa nasaha kwa madktari wenzake juu ya matumizi sahihi ya vifaa.




Comments