
Ameyasema hayo huko
katika katika ziara ya kuwatenbea wajasiriamali na wafanyabiashara wadogowadogo
wa mkoa wa Kusini Pemba kuona juhudi
na changamoto zao na kuangalia njia ya kuwasaidia kupitia mikakati na
malengo ya SMIDA.
Mwenyekiti huyo amesema sio jambo rahisi kuweza kuwasaidia
wajasiri amali mmoja mmoja bali SMIDA itakaa na kufanya uchambuzi kwa ajili
ya kuwaendeleza kielimu na kujaribu kuwatafutia mikopo itakayosaida
maendeleo ya shughuli zao .
Aidha mkurugenzi mkuu wa SMIDA Abdulhamid Idrissa Haji amesema
katika mikakati yao wataanza kuwawezesha
wale walianza vizuri kwa kuzalisha bidhaa zenye ubora kwa kuwatafutia
soko na kuerekebisha baadhi ya miundombinu yao iliyoharibika .
Nao baadhi ya
wajasiriamali hao wameiomba SMIDA kuwapatia wataalamu vitendea kazi na safari
za mafunzo ili kupata uelewa zaidi wa uzalishaji wa bidhaa bora .
Na mwandishi wetu.
Comments